Friday 18 March 2016

MASKINI MTOTO HUYU AZALIWA BILA PUA!!!!


Tukio hili la mtoto anaezaliwa bila kuwa na pua huyokea mara chache sana ambapo kati ya watoto milioni 197 basi humkumba mtoto mmoja.Je mtoto huyo anaishi vipi?

Mtoto huyo Eli,alizaliwa katika eneo la Alabama nchini Marekani mnamo tarehe 4 mwezi wa tatu.Mara baada ya madaktari kumkabidhi mtoto huyo mama,mara moja mama yake aitwae Brand MvGlathery aligundua kuwa mwanae amezaliwa bila kuwa na pua.Aliamua kumpeleka katika hospitali ya 'USA Children's and women's Hospital in mobile' iliyoko pale pale Alabama ili kuona wataalamu wanaoweza kumsaidia mwan
ae. Aliweza kupumua bila shida baada ya kutoka hospitalini pale.

Mama yake amekuwa karibu sana na madaktari kuhakikisha kuwa anapata maelezo sahihi ya namna ya kumtunza vema mtoto huyo.
Tukio kama hili liliripotiwa kwa mara ya kwanza mwaka 1931 na linajulikana kitaalamu kama *Congenital Arhinia*

Inaweza kuwa ni ngumu kuishi kwa hali hii kuelekea utu uzima lakini kuna watoto wameweza kukua wakiwa na hali hii hadi kuwa watu wazima.Mama wa mtoto huyo amekuwa karibu sana na wazazi wa watoto wengine waliozaliwa bila pua na kuweza kukua vema hadi ukubwani licha ya kupata changamoto ya mfumo wa upumuaji.Mama huyo anasema hii imemsaidia sana kuweza kupata taarifa muhimu pia ya namna ya kumlea mtoto wake.

Yuko sawa kwa hali aliyonayo.Pia kunabnjia mbafala ya kumfanyia upasuaji ili kumwekea umbo la pua yaani pua bandia kwa hiyo mama yake analitumainia hilo.Mama yake anasubiri aje aamue mqenyewe ukubwani kama anahitaji pua bandia ama la.
     
           "Hadi pale atakapohitaji pua bandia,sisi hatutafanya lolote lile,tutasubiri uamuzi wake pale atakapoweza kuwa na maamuzi yake mwenyewe"

Alimalizia mama wa mtoto huyo.


Kama umeoendezwa nayo waweza share
Karibu tena kwenye ukurasa huu.

No comments:

Post a Comment