Wednesday 16 March 2016

MWANAMKE MIAKA 62 AOLEWA NA KIJANA WA MIAKA 9!!!!!


Mvulana mwenye umri wa miaka 9 anaejulikana kama Saneie Masilela amekuwa mume mdogo zaidi duniani baada ya kumwoa mwanamke mwenye umri wa miaka 62 ambaye alimchumbia tangu mwaka jana.

Akiwa ndani ya suti yake ya kupendeza mvulana huyo mdogo aliunyanyua mkono wa Bi kizee huyo ambae ni mchumba wake,Helen Shabangu mwenye watoto  watano  na kvisha pete ya ndoa.Watoto wa mama huyo wana umri kati ya miaka 28 na 35.
Mvulana huyo alisema kuwa aliamua kumuoa kabisa baada ya uchumba ili iwe rasmi lakini majirani zake wa vijiji vya Ximhungwe eneo la Mpulanga wanaona kama ni uchizi.
Sherehe ya harusi hiyo ilifanyika mbele ya mume qa zamani wa mwanamke huyo,Alfred Shabangu ,66,ambae pia alihudhuria sherehe za uchumba wao mwaka uliopita.

"Watoto wangu wana furaha sna na ndoa hiina hawana matatizo kwa mimi kuolewa na mvulana huyu mdogo,pia sijali watu wanasema nini juu ya hili."Alisema mwanamama huyo.

Mume huyo mdogo duniani alisema
         "Nilimwambia mama yangu kuwa nahitaji kuoa na kiukweli nilikuwa nahitaji sana.Nina furaha  kumuoa Helen,nampenda lakini nitahakikisha narudi shule na kusoma kwa bidii.Nitakapokuwa mkubwa nitaoa mwanamke wa umri wangu.Nimechagua yeye kwa kuwa sikai nae muda mwingi,huwa nakutana nae eneo ambalo mama yangu anafanyia kazi.“

Mama wa kijana huyo nae alikuwa na ya kuongezea
          "Mwanangu Sanele alikuwa nsawanna mwenye furaha kwa sababu aliitaka ndoa hii na hakuwa na aibu hata kidogo.Alifurahi sana kiasi kwamba alihitaji tena kusherehekea.Wati wengi waliniuliza je wataishi pamoja?Watalala pamoja?Je watapata watoto pamoja?Niliwajibu kuwa baada ya ndoa kila kitu kitakwenda kama kawaida,hakunabkinachobadilika."

Je mnakubaliana na ndoa hii ya ajabu??????

Share tafadhari kama umeipenda.

Asante kwa kuingia ukurasa huu karibu sana kwa habari tamu tamu.

         

No comments:

Post a Comment