Friday 24 June 2016

WAZIRI MKUU WA UINGEREZA AJIUZULU....

Wananchi wa Uingereza wameupitisha mswada wa kujitoa umoja wa ulaya hatua iliyopelekea WAZIRI MKUU kujiuzulu.

Hii ndo inaitwa UKOMAVU WA DEMOKRASIA ambao unapaswa kuigwa na mataifa ya kiafrika ambayo kuna ukandamizahi mkubwa wa demokrasia

Wednesday 8 June 2016

BIONIC MAN-Roboti aliekuwa na hisia na kutenda kama mwanadamu.

Bionic man ni roboti wa kwanza duniani ambaye ametengenezwa akiwa na uwezo wa kuongea,kutembea na kupumua.Ingawa si mwanadamu lakini pia roboti huyu ana moyo wa bandia
Wataalamu wa mambo ya robot Rich Walker na Mathew Godden wa kampuni ya shadow robot ndio walioifanya kazi hii ya kumtengeneza robot huyu aitwae bionic man.
"Kazi yetu ilikua kukusanya sehemu mbali mbali za mwili ikiwa ni pamoja na organ za bandia,miguu,macho ,kichwa kwa muda wa wiki 6 na kuvitumia kutengeneza bionic man"walker alieleza alipokua akihojiwa na livescience
Anasema kazi hiyo haikua rahisi kwani hawakua na binadamu bali walitengeneza kitu ambacho kitafanana na mwanadamu.

MAANA YA FUNGA(SAUMU) NA BARAKA ZAKE


Maana ya funga (Saum)
MAANA ya kufunga (saum) ni kujizuilia. Neno Saumu kwa maana ya kujizuilia linaweza kutumika katika kujizuia kufanya jambo lolote la kawaida mtu alilozoea kulifanya. Katika Qur'an tunafahamishwa kuwa Bibi Maryam baada ya kumzaa Nabii Issa (a.s.) alijizuia (alifunga) ili asiseme na mtu neno lolote juu ya mtoto wake.
"...Na kama ukimwona mtu yoyote (akauliza habari za mtoto huyu) sema: Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwingi wa Rehema ya kufunga, kwa hiyo leo sitasema na mtu". (19:26).
Katika Uislamu kufunga (saumu) ni kujizuilia kula, kunywa, kuvuta sigara, kuingiza kitu chochote katika matundu mengine mawili kama vile pua na masikio, kujizuia na kujamii, kujitoa manii kwa makusudi au kwa matamanio na kujizuia kujitapisha kwa ajili ya Allah (s.w.), kwa kipindi cha kati ya Al-fajri ya kweli mpaka kuingia magharibi. Hii ndio maana ya nje ya Saumu katika Uislamu.
Kufunga katika Uislamu kuna maana ya ndani zaidi, ambayo kama haikufikiwa, kuzuilia kufanya vitendo hivyo vilivyoelezwa hakutakuwa na maana yoyote kwa mfungaji.
Kufunga kwa maana ya ndani ni pamoja kujizuilia kutenda maovu yote yaliyokatazwa na Allah (s.w). Ili saumu ya mfungaji iwe na maana na yenye kufikia lengo, hana budi kukizuilia (kukifungisha) kila kiungo chake cha mwili - macho, ulimi, masikio, mikono na miguu- pamoja na fikra na hisia zake na matendo aliyokataza Allah (s.w.).
Funga ya macho ni kujizuilia na kuangalia aliyoyakataza Allah (s.w.); Funga ya ulimi ni kujizuilia na mazungumzo yote aliyoyakataza Allah (s.w.) kama vile kusengenya, kusema uwongo, kugombana na kadhalika, funga ya masikio ni kujizuia kufanya yale yote aliyoyaharamisha Allah (s.w.); funga ya miguu ni kujizuilia na kuendea yale yote aliyoyakataza Allah (s.w.) funga ya fikra na hisia ni kujizuia na fikra na dhana mbaya ambazo zinampelekea kuvunja amri na makatazo ya Allah (s.w.). Ni katika maana hii Mtume (s.a.w.) anasema katika Hadithi zifuatazo:
Abu Hurairah amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Yule ambaye haachi kusema uwongo na haachi kufanya vitendo viovu, Allah hana haja na kuona kuwa anaacha chakula chake na kinywaji chake (yaani Allah (s.w.) hana haja na funga yake. (Bukhari).
Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Ni wangapi wanaofunga lakini hawana funga ila kukaa na kiu tu ni wangapi wanao swali usiku ambao hawana swala ila huambulia kupoteza usingizi tu. (Darimi).
Hadithi hizi zinatuthibitishia kuwa ufungaji usioambatana na kujizuia na mambo maovu na machafu, haumpatii mfungaji faida yoyote.
Umuhimu wa funga katika Uislamu
Funga ya Ramadhani ni miongoni mwa nguzo za Uislamu na ni faradhi kwa Waislamu kama inavyobainika katika aya ifuatayo:
Enyi mlioamini! Mmeamrishwa kufunga (saumu) kama walivyofaradhishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu. (2:183)
Kama ilivyo katika nguzo nyingine za Uislamu, mtu atakapoivunja makusudi nguzo hii hatabakia kuwa Muislamu japo atajiita Muislamu na watu wakaendelea kumwita hivyo. Katika Hadithi iliyopokelewa na Ibn Abbas, Mtume (s.a.w.) amesema:
Kuna viungo vitatu vinavyomuunganisha Muislamu na dini ya Uislamu na yeyote yule atakayevunja kiungo kimoja katika hivi atakuwa amekana Uislamu na kuuawa kwani ni halali. Viungo hivi ni: Kushuhudia kuwa hapana Mola ila Allah, Kusimamisha Swala tano na kufunga mwezi wa Ramadhani.
Katika Hadithi nyingine Abu-Hurairah (r.a.) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w.) amesema:
Yeyote yule atakaye acha makusudi kufunga siku moja ya mwezi wa Ramadhani, hawezi kuifidia siku hiyo hata akifunga kila siku katika umri wake wote (uliobakia). (Abu-Daud)
Funga ni ibada maalum iliyo muhimu sana katika kumuandaa mja kuwa mcha Mungu kwa kule kukataa kwake matamanio ya kimwili. Hivyo Allah (s.w.) kwa ukaribu wake ameahidi malipo makubwa kwa wenye kutekeleza ibada hii ili iwe motisha kwao ya kuwawezesha kutekeleza ibada hii kwa hima kubwa na kwa ukamilifu unaotakikana kama tunavyojifunza katika Hadithi zifuatazo:
Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Mwenye kufunga Ramadhani akiwa na imani na akawa na matumaini ya kupata malipo kutoka kwa Allah dhambi zake zote zilizopita husamehewa, Na mwenye kusimama kwa swala (tarawehe) katika mwezi wa Ramadhani akiwa na imani na matumaini ya kupata malipo (kutoka kwa Allah), dhambi zake zote zilizopita zitasamehewa. Na yule atakayesimama (kwa swala) katika usiku uliobarikiwa (Lailatul-Qadri) akiwa na imani na matumaini ya kupata malipo kutoka kwa Allah (s.w.) dhambi zake zote zilizotangulia zitasamehewa. (Bukhari na Muslim).
Pia Abu-Hurairah ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Kila amali njema anayoifanya mwanaadamu italipwa mara kumi (Al-Qur'an 6:160) mpaka kufikia mara mia saba (Al-Qur'an 2:261). Allah (s.w.) amesema:
Ila kufunga kwa sababu funga ni kwa ajili Yangu, na ni mimi mwenyewe nitakayeilipa. Mwenye kufunga anakata matamanio yake ya kimwili na anaacha chakula kwa ajili yangu. Kwa mwenye kufunga kuna furaha mbili, furaha moja anaipata wakati wa kufuturu na nyingine wakati atakapokutana na Mola wake. Na hakika harufu ya mdomo wa mwenye kufunga ni bora mbele ya Allah (s.w.) kuliko harufu ya miski. Na funga ni ngao. Kwa hiyo atakayefunga miongoni mwenu hataongea maneno ya upuuzi wala hatagombana. Kama itatokea achokozwe na yeyote, au mtu atakakupigana naye, na aseme: Nimefunga. (Bukhari na Muslim).
Vile vile Mtume (s.a.w.) katika kusisitiza umuhimu wa funga ya Ramadhani alitoa khutuba mwishoni mwa mwezi wa Shaaban kama ilivyonukuliwa katika hadithi ifuatayo:
Salman al-Farisy ameeleza: Mtume (s.a.w.) alituwaidh mwisho mwa siku ya Shaabani akasema: Enyi watu! Hakika umekujieni mwezi mtukufu, mwezi uliobarikiwa, mwezi ambao ndani yake kuna usiku uliobora zaidi kuliko miezi elfu moja. Allah (s.w.) amefaradhisha kufunga katika mwezi huu na kusimama (kwa swala ya tarawehe) katika mausiku yake ni sunnah. Atakayetekeleza kitendo kizuri kisicho faradhi atapata ujira wa mtu aliyetekeleza kitendo cha faradhi katika miezi mingine, na yule atakayetekeleza kitendo cha faradhi atapata ujira wa mara 70 wa ujira wa kitendo hicho katika miezi mingine. Na ni mwezi wa subira, na ilivyo, subira malipo yake ni pepo. Na ni mwezi wa kuhurumiana na mwezi ambao mahitaji (mapato) ya muumini huongezwa. Atakayetoa futari kwa mwenye kufunga katika mwezi huu kuna kusamehewa dhambi zake na kuwekwa huru na moto, na atapata malipo sawa na ya yule aliyefunga bila ya yeye kupunguziwa chochote. Tukauliza: Ee Mtume wa Allah! Hakuna yeyote kati yetu mwenye uwezo wa kumfuturisha mtu aliyefunga. Alijibu Mtume: Allah atamlipa yule mwenye kumfuturisha aliyefunga kwa funda la maziwa, au tende moja au funda la maji. Na yule anayekidhi haja ya mtu Allah atamnywesha kutokana na Birika (Kawthar) langu na hatakuwa na kiu mpaka atakapoingia peponi.
Na (Ramadhani) ni mwezi ambao mwanzo wake kuna kurehemewa, katikati yake kuna kusamehewa na mwisho wake kuna kuachwa huru na moto. Na yule atakayempunguzia kazi mtumwa (mfungwa vita) wake, Allah atamsamehe, na atamuacha huru na moto.
Historia ya kufunga
Funga, kama ilivyo katika ibada nyingine kama tulivyoona katika kusimamisha swala na kutoa zakat, imetekelezwa na Mitume wote pamoja na umma zao. Allah (s.w.) ametukumbusha hili wakati alipotupa amri ya kutekeleza ibada hii maalum, kama tunavyorejea katika Qur'an:
Enyi mlioamini! Mmeandikiwa (mmefaradhishiwa) kufunga kama walivyofaridhishiwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu. (2:183)
Katika historia tunajifunza kuwa, kila Mtume alipoondoka, baada ya kipindi kupita, watu waliacha mafundisho yake na kuingia katika ushirikina. Lakini bado tunakuta funga, japo si katika madhumuni na asili yake iliyoachwa na Mitume wa Allah (s.w.), imebakia katika jamii za kishirikina kwa kipindi chote cha historia. Hebu tuangalie mifano michache ya dini za ushirikina ambapo funga, kwa maana ya kushinda na njaa na kiu, imekuwa miongoni mwa ibada muhimu za dini hizo.
Jamii ya Nabii Ibrahim
Nabii Ibrahim (a.s.) aliinuliwa katika jamii ya washirikina. Walikuwa wakiabudu jua, mwezi, nyota na masanamu chungu nzima waliyoyachonga wenyewe. Pamoja na ushirikina wao huo walikuwa wakifunga siku 30 mfululizo katika kila mwaka kwa heshima ya mwezi
Wahindu (Hinduism)
Dini ya Kihindu ni miongoni mwa dini za kishirikina katika bara la India. Katika dini hii funga, ni kitendo kilichosisitizwa sana japo si lazima, katika siku maalum kama vile kupatwa kwa jua, kumbumbuku ya kuzaliwa mwanzilishi wa dini yao na kadhalika. Funga kwao ni kujizulia na kula na kunywa kuanzia alfajiri mpaka saa tisa mchana.
Mayahudi (Judaism)
Dini ya Kiyahudi ni dini waliyoibuni Mayahudi baada ya Nabii Musa (a.s.) ambapo walimfanya Uzairi mwana wa Mungu. Pamoja na hivyo wachaji wa Kiyahudi walikuwa wakifunga Alhamisi na Jumatatu kama kumbukumbu ya kwenda na kurudi kwa Nabii Musa (a.s.) katika safari yake ya Sinai kwenda kuchukua Taurati. Kutokana na kumbukumbu ya historia, Nabii Musa alikwenda kwenye mlima Sinai siku ya Alhamisi na kurejea siku ya Jumatatu baada ya siku arobaini kupita.
Pia Mayahudi hufunga kwa saa 24 katika kila mwezi 10 Muharamu, kwa kumbukumbu ya siku Wanaisraili ( Mayahudi) walipookolewa na Allah (s.w) kutokana na udhalimu wa Firaun. Siku hii ambayo hata Waislamu wamesuniwa kufunga huitwa siku ya Ashuurah.
Pamoja na funga hizi, pia Mayahudi wana tabia ya kufunga mara kwa mara kulingana na haja. Kwa mfano mtu anaweza kuamua kufunga siku kadhaa kama kumbukumbu ya matukio fulani katika maisha yake, au anaweza kufunga funga kama kitubio cha madhambi yake, au anaweza kufunga wakati akiwa na matatizo ili kupata huruma ya Mungu.
Ukiacha siku ya Ashuura ambapo funga huchukua saa 24, funga za Mayahudi huanza alfajiri na huishia pale inapojitokeza nyota ya kwanza usiku.
Wakristo
Dini ya Ukristo imebuniwa baada ya Nabii Issa (a.s.). Katika dini hii Nabii Issa (a.s.) amefanywa mwana wa Allah (s.w.) na kwamba yeye ndiye mkombozi wa Wakristo. Pamoja na hivyo, Wakristo wanakiri kuwa kufunga ni kitendo cha uchaji - katika dini yao. Wakristo wa mwanzo walikuwa wakifunga siku 40 mfululizo kasoro siku za Jumapili kama kumbukumbu ya siku zile alizofunga Yesu (Nabii Issa a.s.) kama inavyobainishwa katika Biblia.
Historia inatuonyesha vile vile kuwa funga hizi za Washirikina zimetofautiana sana katika mfumo na funga ya Kiislamu aliyoiamrisha Allah (s.w.). Ambapo Waislamu wakifunga hujizuia kula, kunywa na kujamii mchana kutwa kuanzia alfajiri mpaka kuchwa kwa jua, funga za washirikina zilichukua mifumo mbalimbali. Wengine walijizuilia kula na kunywa tu lakini waliendelea kujamii, wengine walijizulia kunywa na kula kuanzia alfajiri mpaka saa 9 alasiri, wengine walijizulia kula aina fulani tu ya chakula kama vile nyama, wengine walijizulia kwa kunywa tu maji yaliyochanganywa na chumvi au maji ya ndimu, na kadhalika.

Friday 3 June 2016

BONDIA MAARUFU MUHAMMAD ALI AFARIKI DUNIA.



Aliekuwa bondia maarufu duniani,Muhammad Ali amefariki kwa mujibu wa msemaji wa familia yao.Ali amefariki akiwa na umri wa miaka 74.

Bingwa huyo wa mara tatu wa dunia alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa tangu mwaka 1984 miaka mitatu baada ya kustaafu mchezo wa masumbwi.

Siku moja kabla ya kukubwa na umauti,Ali,alipelekwa hospitali ya Phoenix,Arizona akiwa na matatizo ya upumuaji.Tatizo hili lilipelekea matatizo ya neva za fahamu yaliyoathiri pia mfumo wake mzima wa upumuaji.

Mazishi yake yatafanyika katika mji aliozaliwa wa Louisville,Kentucky.
 
         "Familia ya Ali inapenda sana kuwashukuru sana kwa mawazo,sala na sapoti mliotuonyesha kwa kipindi chote cha kumuuguza Ali"Alimalizia msemaji wa familia.

Rest in peace MUHAMMAD ALI,THE BEAST


Asante kwa kutembelea ukurasa huu.

Share kadili uwezavyo.

Wednesday 18 May 2016

KIJANA WA MIAKA 31 AZAMIA KATIKA PENZI LA BIBI WA MIAKA 91.


Kila mmoja anaamini kuwa umri ni namba tu katika mapenzi.Kama unampenda mtu umri wake hauna nafasi katika mapenzi yenu.Je ni kweli imani hii ina ukweli ndani yake katika kila penzi??

Kutana na Kyle Jones 31,ambaye yuko katika penzi la dhati na bibi kizee mwenye umri wa miaka 91 anaemzidi takribani miaka 60 kijana huyo.Unaweza kusema Kyle yuko katika mapenzi na mtu ambae anapaswa kumwita BIBI.

Kyle anasema anampenda sana MPENZI BIBI huyo ambae tunaweza sema SUGAR BIBI kwa lugha ya vijana wa town.

SHARE NA WENZIO WAPATE HABARI HII.

@viroshare

Wednesday 11 May 2016

IJUE NYOTA YAKO NA TABIA ZAKE


Unajimu au astrolojia ni elimu juu ya uhusiano kati ya nyota na maisha ya binadamu duniani. Wanazuoni wa unajimu wanaeleza ya kwamba nyota zinaathiri maisha ya watu na matukio kama amani, vita au maafa. Mahusiano haya hayajaweza kuthibitishwa na sayansi ya fizikia au sayansi nyingine. Alama za nyota 12 ni msingi wa falsafa hii ya unajimu.
Astrologia imekuwa ikitumika kwa miaka mingi lakini siku zote imekuwa ikipata upinzani mkubwa toka kwa wana sayansi.
Astrolojia ina misingi tokea enzi za zamani wakati sayansi ilipokuwa ya chini na imani za kiroho na kiungu zikiwa za kiwango cha juu katika jamii nyingi.
Baadhi ya tafiti zilizofanywa kuchunguza usahihi wa astrolojia unaonyesha kuna usahihi wa asilimia kama 3o tu. Hii si haba,kuna ukweli basi katika hili japo bado kuna upinzani mkubwa toka katika ulimwengu wa sayansi ya kisasa.
[Soma pia: Madhara ya Mwezi Katika Hisia na Tabia za Binadamu:Kuna Ukweli? , Nyota na Kazi Zenye Mafanikio ]
Tabia Za Watu Na Alama Za Nyota
Alama za nyota zinabashiri tabia na haiba ya binadamu katika dunia. Mpangilio au nafasi ya sayari katika mzunguko wake angani unaaminika kuleta athari kwa binadamu na matukio katika dunia.
Kuna alama 12 za kiastrolojia. Kila moja ina mvuto wa nguvu wa kipekee toka katika nyota.
Alama hizi ni kama ifuatavyo:

1. Samaki (Pisces):Feb 19 – Machi 20
2. Kondoo (Aries): Machi 21 – Aprili 19
3. Ng’ombe (Taurus): Aprili 20 – Mei 21
4. Mapacha :(Gemini ): Mei 22 – Juni 20
5. Kaa(Cancer): Juni 21 – Julai 22
6. Simba (Leo): Julai 23 – Agosti 22
7. Mashuke (Virgo):Agosti 23 – Sept 22
8. Mizani (Libra): Sept 23 – Okt 22
9. Ng’e (Scorpio): Okt 24- Nov 21
10. Mshale (Sagittarius): Nov 22- Des 21
11. Mbuzi (Capricorn):Des 22 – Jan 19
12. Ndoo (Aquarius):Jan 20 – Feb 18

Makundi Ya Alama Za Nyota:
Alama hizi 12 za nyota zinagawanyika katika elementi 4 zijulikanazo kama:
Moto: Yenye matamanio ya mafanikio au makuu,dadisi
Maji: Yenye kubadilika na yenye uwezo wa ufahamu wa ndani
Hewa: Imara na yenye kukuza au kuendeleza
Udongo: Yenye elimu au uwezo wa kutambua na yenye kuhamasisha
Hizi ni elementi nne zinazoongoza astrologia. Kila kimojawapo kinabeba tabia fulani.

Alama hizi 12 za nyota zimegawanyika kama ifuatavyo:
Moto : Kondoo, Simba,Mshale
Maji: Ng’e, Samaki, Kaa
Hewa: Mapacha, Mizani, Ndoo
Udongo: Ng’ombe,Mashuke,Mbuzi

ZIFUATAZO NI NYOTA MBALI MBALI NA TABIA ZAKE







SHARE KADRI UWEZAVYO NDUGU. .ASANTE KARIBU TENA KWA HABARI ZA KIPEKEEE

Wednesday 4 May 2016

TANZANIA YAONGOZA KWA UKUAJI WA UCHUMI EAC

Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu zaidi cha ukuaji wa uchumi wake mwaka huu katika kanda ya Afrika Mashariki na kati.
Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la fedha la kimataifa - IMF.
Katika ripoti yake iliyotolewa hii leo Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu cha ukuaji wa uchumi wake wa asilimia 6.9% mwaka wa 2016.
Kasi hiyo ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania ni ya pili tu nyuma ya Ivory Coast baina ya mataifa ya Kusini mwa jangwa la Sahara .
Ivory Coast inatarajiwa kukuwa kwa kasi ya asilimia 8.5%.
Katika kanda ya Afrika Mashariki ,uchumi wa Kenya ndio wa pili kwa kasi ya ukuaji kwa asilimia 6%.
IMF hata hivyo inasema kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi kusini mwa jangwa la Sahara unatarajiwa kupungua kwa mwaka wa pili mfululizo kutokana na kudorora kwa viwango vya uzalishaji na hivyo uwekezaji.
Kwa mujibu wa shirika la fedha la kimataifa - IMF, eneo hilo linakadiria kushuka kwa ukuwaji wa uchumi kwa asilimia 3 mwaka huu.
Kiwango hicho ni cha chini kabisa kuwahi kushuhudiwa katika miaka 15.
Mataifa yanayotegemea mapato yanayotokana na mafuta ndiyo yalioathirika zaidi kama vile Nigeria na Angola.
Aidha Zambia pia imeathirika vibaya kutokana na ukosefu wa soko la kimataifa la shaba yake.
Ripoti hiyo inaitaja Afrika Kusini kama moja ya mataifa ambayo kiwango chake cha ukuaji kimedorora kwa kiasi kikubwa mno.
Katika orodha ya mataifa yanayotarajiwa kuwa na kiwango cha juu cha ukuaji Kusini mwa jangwa la sahara Ivory Coast ndio inayoongoza.
Orodha ya mataifa ya kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara na viwango vya kasi ya ukuaji wa uchumi 2016.
1. Ivory Coast 8.5%
2. Tanzania 6.9%
3. Senegal 6.6%
4. Kenya 6%
5. Zambia 3.4%
6. Nigeria 2.3%
7. Afrika Kusini 0.6%

Source:bbc

Tuesday 3 May 2016

JINI MAHABA NA NAMNA MAJINI WANAVYOINGIA KATIKA MAISHA YA BINADAM




Majini ni viumbe ambao wameumbwa kwa Moto na walikuwa wakiishi duniani kabla ya binadamu miaka Milioni nyingi iliyopita.
Viumbe hawa wana tabia kubwa mbili;
Yaani ya kibinadamu kwa maana wanakuwa wanafanya mapenzi, wanazaa na wanakufa.
Tabia nyingine ni ya Kimalaika ambayo ni kwamba wana uwezo wa kujigeuza katika umbo lolote wanalotaka na vile vile wanaruka na kwenda wanakotaka au kupita wanakotaka bila kutumia chombo chochote.
Taifa la Majini limegawanyika katika makabila Milioni Sabini na mbili (72,000,000) na wana uwezo wa kujifunza lugha yeyote wanaoitaka.
Idadi ya Majini ni kila Binadamu mmoja kuna Majini 300 na wanaishi katika Majumba yetu, kwenye Miti, Majangwani, Kwenye Mapango na Sehemu zenye Misitu Mikubwa.
Majini wako katika aina Mbili (2); Maruhani na Mashetani.
Maruhani ni Majini wema ambao wanamtii Mwenyezi Mungu na wanawasaidia Binadamu katika mambo mengi.
Mashetani ni Majini Waovu ambao ni wakorofi na wanawaletea Watu madhara na Matatizo mara kwa mara.

Baba wa Majini anaitwa JANN ambaye kimaumbile yeye ana tofauti ndogo na wenzie kwamba yeye ameumbwa kwa ulimi wa Moto.
Pamoja na mambo mengi wanayoyafanya Majini na kujihusisha na binadamu, Majini vilevile wanafanya kazi za Malaika hasa zile za mambo ya kupeleka Habari na kuwalinda Binadamu, mambo ya doria za Angani. Kazi hizi siyo zao lakini kwa vile wanapenda kuiga mambo basi huiga hata kazi ambazo siyo zao.
Majini na Binadamu wana sifa zinazofanana kwani wote wana akili na wote watahesabiwa siku ya Kiama na watazawadiwa kwa mema yao na maovu yao, wote wanakula na kuzaa.
Kama ilivyo, kuna wataalamu wa Kijini wenye fani sawa na Wataalamu wa Kibinadamu wenye kufanya kazi zinazofanana.
Tofauti kubwa iliyopo kati ya Majini na Binadamu ni kwamba; Majini hawana maumbile maalum na wana uwezo wa kujibadilisha katika maumbile mbalimbali ingawa wengi wa Majini wapo katika maumbile ya paka, nyoka na ndege.
Binadamu wao wana umbile maalum ambalo halibadiliki.
Majini wana uwezo wa kuwaingia Binadamu wakati Binadamu hawana uwezo wa kuwaona Majini isipokuwa kwa ufundi maalum.

Namna Majini wanavyowaingia Binadamu iko katika njia tatu:-
1. Njia ya kwanza (1): ni kama Remote Control; Hii inamfanya yule aliyedhibitiwa kuweza kuelewa au kuwa na fahamu zake lakini anakuwa hawezi yeye mwenyewe kuudhibiti mwili wake na anasema yale anayotaka yule Jini.
2. Njia ya Pili (2); Jini humwingia Binadamu ndani ya utosi na kuingia katika Mfumo wa Damu. Hii inamfanya yule Binadamu kupoteza fahamu na anakuwa haelewi kabisa kinachoendlea na anafanya yote anayotaka yule Jini.
3. Njia ya Tatu (3) ni ile ya Jini kukaa nyuma ya Binadamu. Njia hii humfanya yule Binadamu anakuwa hapotezi fahamu ila anakuwa hawezi kufanya lolote na mwili wake.
{mospagebreak}

Majini vilevile wana uwezo wa Kusafiri kwa kasi ya upepo bila kutumia chombo chochote; Binadamu hana uwezo huo isipokuwa kwa msaada wa Majini.
Hiyo ni kusema kwamba mambo yote yanayofanywa na Wachawi na Wanga hayawezekani isipokuwa kwa msaada wa Kijini.
Jambo la muhimu ni kwamba pamoja na uwezo mkubwa walionao Majini, Wanadamu wana uwezo wa Kumtawala na Kumdhibiti Jini na vivyo hivyo Majini nao wanaweza kumtawala na kumdhibiti Binadamu wote kwa kutumia utaalamu maalum.
Wako Majini wa kila Dini na kila Kabila, na kuna watu wanaofuga Majini kwa kujikinga, na kwa kuboresha kazi zao au kujipatia utajiri. Pia kuna watu wanaofunga ndoa na Majini kwa kutumia utaalamu au kwa hiari za Majini hao.
Wabaya wa Majini ni Mashetani ambao wengi hawana Dini na ndio wanaoharibu mimba za Wazazi na kufanya mapenzi na watu usingizini bila hiari zao.
Kuepuka usichafuliwe kimapenzi, kabla ya kulala piga Bismillahi kwa Muislamu au taja jina la Yesu mara tatu kwa Mkristo.

MAUMBILE YAO YAKOJE?

· Majini wana maumbile makuu manne (4);
· Wanakuwa katika maumbile ya Nyoka.
· Wanakuwa katika maumbile ya Nge.
· Wanakuwa katika maumbile ya Mbwa.
· Wanakuwa katika maumbile ya Paka (Mweusi).
· Kuna Majini wengine hawana maumbile yeyote na hawa shughuli yao ni kuruka hewani kuzunguka huku na kule na husafiri mbali kwa mara moja yaani kufumba na kufumbua.

SURA ZA MAJINI NA MASHETANI:
Majini sura zao ni za kutisha na mfano wake ni kama Matunda ya Mti wa Zaqum ambao unatoa matunda yenye sura mbaya na yanayofanana na mawe.
Majini wanakuwa na mkutano kila siku nyakati za kuchomoza na kuzama Jua na nyakati hizo ndizo ambazo wanafanya maasi yao.
Fitna na Maasi yao mengi wanafanyia upande wa Mashariki.
Majini vilevile wanaweza kujigeuza kama mbwa mweusi au paka mweusi kwa sababu Majini wanapenda Rangi Nyeusi kwa sababu ya kiza.

WANAKULA NINI?
Majini wao wanakula mifupa na mavi ya farasi. Hivyo ni vyaluka vyao vikuu pamoja na kwamba wengine wanakula Moshi (Ubani) na wengine wanapenda kunywa damu.
Wanapokula au kunywa, wao hutumia mkono wa kushoto na Majini wazuri ndio ambao wanakula mifupa mizuri na kuwaachia mifupa mibaya na uchafu Majini wabaya au Mashetani.

JE MAJINI WANAZAA?
Majini wanaoa na kuongezeka kama tulivyo Binadamu na huzaana kwa wingi sana.
Katika wao kuna wale wanaokula na kuoana na kuna wale ambao hawafanyi hayo.
Binadamu Mwanamume ana uwezo wa kumuoa Jini Mwanamke na Jini wa Kiume ana uwezo wa kumuoa Binadamu Mwanamke pamoja na kwamba ndoa inayotambulika na Mwenyezi Mungu ni ya kiumbe kwa kiumbe yaani Binadamu kwa Binadamu na Jini kwa Jini.
Huyu ni JINI MAHABA wa Kike anaitwa SUCCUBI huwajia wanaume na kufanya nao Mapenzi
Jini Mahaba wa kiume akiwa Kazini ni hatari sana hawa

Tuesday 26 April 2016

UNYAMA WA KUTISHA,MFANYAKAZI WA NDANI AUNGUZWA NA MAJI YA MOTO SEHEMU ZA SIRI!!!

Jaman mume afumaniwa na house girl mke akawamagia maji ya moto, ila mke hakufanya feya kw house girl cz anaonyesh ni mdogo huyo mam hasira angemaliza kw mume wake sio kw house girl hana makosa hako kanaonyesha ni kadogo San unawez kukuta alimbaka angesubir amuuliz maswal kwanz thn amrudishe kwao...

Huu ni unyama wa kutisha sana haijalishi ni kosa gani wahusika wamefanya.


UTU KWANZA NDOA BAADAE.

Sunday 24 April 2016

MAMBO 10 YA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHAGUA MCHUMBA AU MPENZI MPYA❤❤


Wengi wamejikuta wakiitwa wahuni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na makundi ya wanaume au wanawake. Hata hivyo wachunguzi wa masuala ya mapenzi wanasema idadi kubwa ya wapenzi si kigezo sahihi cha kupima tabia ya mtu na kumhusisha na uhuni.
Watalaam hao wanataja safari ya kupata chaguo halisi la mwanaume/mwanamke wa maisha ndiyo inayowaponza wengi kiasi cha kujikuta wameingia katika kashfa ya kuwa na uhusiano na dazeni ya wapenzi.
Wanasema msichana/mvulana anayeingia katika uwanja wa mapenzi kwa kuwa na hisia za kufanya ngono, hukosa umakini wa nani anafaa kuwa mpenzi wake kutokana na kukosa elimu ya uhusiano kutoka kwa wazazi wake.
Kwa mantiki hiyo, bila upembuzi wa kina, mtu asiye na elimu ya jinsi ya kumpata mpenzi wa kweli hujikuta ameangukia kwa mwanaume/mwanamke asiyemfaa, ambapo baadaye huamua kuachana na huyo na kwenda kwa mwingine kujaribu bahati tena ya kupata penzi la kweli.
Zinatajwa zawadi, hitaji la kusaidiwa kimaisha, mvuto wa kimahaba na mazoea kuwa ni vichocheo vinavyowaangusha wengi kwenye mapenzi na wasiowafaa.
Ukweli ni kwamba mtu aliyenaswa kwa ‘ujinga’, huwa hakatwi kiu ya penzi na mwanaume/mwanamke asiye chaguo sahihi la maisha yake. Hivyo hufikia maamuzi ya kujiingiza katika uhusiano mpya mara 2,3,4,5 na kujikuta wakiambulia wanaume/wanawake wale wale wasio sahihi kwake.
Mwanamnke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Ramla aliwahi kuniomba ushauri, akasema amechoka kuchezewa, maana kila mwanaume anayempata anakuwa si chaguo lake. Lakini kibaya zaidi kuachia ngazi au kutemwa huku akiwa tayari ameshafanya mapenzi na wanaume hao.
Na leo my best friend na mdau wangu mkubwa wa Blog hii  Rayha ametaka kujua vigezo gani vya kuzingatia ili kumpata mume/mpenzi borana mwenye mapenzi ya kweli na ya dhati , hii ameiandika kwenye ukurasa wake wa facebook.
Nia ya swali lake ilikuwa ni kuniomba njia za kumtambua mwanaume mkweli bila kufanya naye mapenzi? Aliuliza hivyo huku akiwa na hoja kuwa wanaume wengi hawako tayari kuwa na uhusiano na msichana bila kufanya naye mapenzi na wakati huo huo huficha tabia zao chafu wakilenga kumnasa wamtakaye.
Binafsi nafahamu kuwa kuna wanawake/wanawake wengi ambao hujiingiza katika mapenzi kwa kutekwa na hadaa za mwili na kujikuta wanacheza mchezo wa kitoto wa pata potea.
Ni madhumuni ya somo hili kufundisha vigezo vya kumpata mwanaume/mwanamke halisi wa maisha, bila kufanya naye mapenzi. Njia hii ina faida kwa pande zote mbili yaani kwa mwanamke na mwanaume kwani kuacha au kuachwa bila kufanya mapenzi ni bora kuliko kuwa muonjaji, tabia ambayo huathiri kisaikolojia na ni hatari kwa afya.
Ifuatavyo ni njia ya kisaikolojia ambayo mwanamke anaweza kutumia kumpata mwanaume mwenye kumfaa bila kufanya naye mapenzi tena ni jibu sahihi la kuondokana na mchezo wa kubahatisha kwa wanaume wanaosaka wapenzi wa kweli na si taksi bubu ambazo mchana huweka namba za njano usiku nyeusi.

KWANZA- Ni ya mwanamke/mwanaume mwenyewe kujifahamu na kufahamu vigezo vya mpenzi anayemhitaji katika maisha yake. Ifahamike kuwa kila mwanaume ana wake na kila mwanamke anaye wake wa maisha pia. Hivyo asiyekufaa wewe anawafaa wengine, kinachotakiwa ni wewe kujitambua kwanza ili umtambue umtakaye.
Wanawake/wanaume wengi hawafahamu wanahitaji wapenzi wa aina gani, hivyo wanajikuta kama watu wanaoingia sokoni bila kujua wanataka kununua nini? Ndiyo maana wengi wameangukia kwa matapeli wa mapenzi, wakachezewe na kuumizwa moyo bure.

PILI- Ni kuketi chini na kuorodhesha vigezo stahili vya mwanaume/mwanamke unayemtaka. Baada ya hapo orodhesha tena kasoro za mwanaume/mwanamke unazoweza kuzivumilia na zile ambazo huwezi kuzivumilia kabisa. Hii inatokana na ukweli kwamba mwanadamu hajakamilika, ana upungufu wake.

TATU- Anza kumsaka kwa kutumia milango ya fahamu. Cha kufanya hapa ni kuruhusu macho yawaone wanaume/wanawake na kuwatathmini kwa maumbile yao ya nje na kisha kupata majibu kutoka moyoni juu ya kuvutia kwao ambako hutambulika kwa moyo kurithika na mwili kusisimka.

NNE - Kuanzisha safari ya kuchunguza tabia za nje na za ndani kivitendo. Hapa suala la ukaribu baina ya mwanaume na mwanamke linahitajika. Msingi unaotajwa hapa ni kujenga mazoea ya kawaida yasiyokuwa na masuala ya kimapenzi na ngono. Kutambuana, dini, viwango vya elimu, kabila na makundi ya marafiki ni mambo ya kuzingatia.
Katika uchunguzi huu mwanamke/mwanaume anayetafuta mpenzi hana budi kupitia na kumlinganisha huyo aliyempata na vigezo alivyojiwekea. Zoezi hili liendane na kuweka alama ya pata kila anapobaini kuwa mwanaume/mwanamke anayemchunguza amepata moja ya vigezo vyake. Lakini pia aweke alama ya kosa kwa kila kasoro anayoivumilia na ile asiyoivumilia.

TANO - Ajipe muda wa kutosha kati ya miezi sita na mwaka kumchunguza huyo mwanaume, kisha aketi chini na aanze kujumlisha alama za vigezo alivyovijiwekea na jinsi mwanaume huyo alivyopata au kukosa.
Ikibainika mwanaume aliyechaguliwa amepata zaidi ya nusu ya alama ya vigezo vilivyowekwa, basi ujue kuwa anafaa. Kuhusu alama chache alizikosa anaweza kusaidia kuzikamilisha polepole wakati wa maisha ya ndoa.
Lakini angalizo kubwa kabisa ni kwamba mwanaume/mwanamke akionekana kuanguka katika kasoro zisizoweza kuvumilia kwa zaidi ya alama tatu. Yaani kwa mfano ni mlevi, mwizi, muongo, mbishi na katika hizo kashindwa 3, huyu hafai, ni vema akawekwa kando kwani huwezi kubeba kero 3 kwa pamoja katika maisha.

SITA - Kusajili mapenzi yenye malengo yanayotekelezeka. Lazima baada ya kuchunguzana kwa kina wapenzi watengeneze muongozo wa mapenzi yao. Wasiwe kama wanyama, lazima mipango ya wapi wametoka walipo na wanapokwenda.
Hata hivyo watalaam wanasema lazima wapenzi wapime umakini wao kwa vitendo. Kama wamekubaliana kuoana, suala la mume kwenda kujitambulisha kwa wakwe na hatua ya kuiendea ndoa ionekane. Usiri usiwepo tena. Kila mmoja amuone mwenzake kama sehemu ya maisha yake na mara zote wasaidiane kwa ukaribu.

SABA - Ni vema ndugu wakashirikishwa ili kuwapa nafasi na wao ya kuamua kama mapenzi hayo ni budi yakaendelea au yakasitishwa. Ni ukweli ulio wazi kwamba licha ya wengi kupuuza maamuzi ya ndugu kwa madai ya kuwa hawana nafasi kwa wapenda nao, lakini uchunguzi unaonesha kuwa wapenzi wengi huacha kutokana na sumu za ndugu hasa pale wanapokuwa wameonesha kutounga mkono uhusiano wa wanaotaka kuoana

NANE - Hatua hii ni ya kuweza kuzungumzia ufanyaji mapenzi, hapa nina maana kama wapenzi wamejizuia kwa muda mrefu na wanahisi kuchoka wanaweza kujadiliana kuhusu hilo na kuamua ufanyaji huo wa mapenzi una lengo gani, kama ni kuburudisha miili basi suala la afya na uzazi salama litazamwe.

TISA - Kutimizwa kwa ahadi ya kuoana ni hatua ya tisa ambayo nayo si busara ikachukua muda mwingi kutekelezeka, kwani ucheleweshaji mwingi wa ndoa nao huvunja moyo na mara nyingine umewafanya wengi kutoaminiana.

KUMI - Kuamua kuwa mwili mmoja kwa kuvumilia na kuwa tayari kukabiliana na changamoto zote za maisha ukiwemo mkwamo na dhiki ambazo huchangia sana ndoa nyingi kuvunjika. Hapa pia ni wajibu wa wanandoa kuchukuliana udhaifu na kusaidia, kuwa tayari kujifunza na kujali zaidi upendo kuliko hisia za mwili ambazo wakati mwingine hudanganya na hivyo kumfanya mwanandoa asivutiwe na mwenzake.
Mwisho ni kwamba kanuni hizi huwafaa watu wazima mapenzi ya kitoto hayawezi kujenga misingi hii imara mara nyingi ni kudanganyana, kuharibiana maisha, kupeana mimba na maradhi.

Saturday 16 April 2016

ROBOTI LENYE HISIA ZA KIBINADAMU LATENGENEZWA CHINA!!!😂


Je unaweza tambua roboti kati ya hawa watu kwa hizi picha ? Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia ya China katika mji mkuu wa Hefei, mashariki mwa China kimezindua roboti kwa jina "Jiajia" ambayo ina uwezo wa mwingiliano na binadamu.

Jiajia ni huyo mwenye mwanamke mwenye nguo nyekundu, anaweza kila kitu ambacho mwanamke anaweza kasoro kubeba mimba tu, lakini hisia za kupenda na kuchukia, hisia za kulala na mwanaume na mengi kama hayo.
Roboti hizo zinauwezo wa kutongoza au kutongozeka, zinaweza kukataa au kukubali inategemea na uwezo wako wa kushawishi.

Bado bei yake haijapangwa, na yapo yanayotengenezwa maalum kwaajili ya Afrika, je yakija Tanzania utanunua?? yakiume pia yatatengenezwa kwaajili ya kazi mbalimbali kama kulima nk.
Watu watabisha lakini mbona wanakula mayai kizungu, kuku za kizungu, sasa kuna ubaya gani mkila na nyapu/zakari za kichina? Au wachina hamuwaamini?

JAMANI MPENZI WANGU

NILIKUWA NA MPENZI MTUNZI:
 George Iron Mosenya SIMU: 0655 727325

Mwanzoni sikumpenda kutoka moyoni, nilimpenda kwa kuwa tu alikuwa mrembo haswa..kwa kifupi nilimtamani tu….yaani nilitegemea akinivulia nguo zake tukashiriki tendo hamu yangu itaisha na nitaachana naye. Ndio ningeachana naye kwa sababusikuona umuhimu wa kudumu na msichana ambaye sijui hata kama nitamuoa. Nilipomwambia tutaoana hakika nilidanganya Alinipenda sana, kadri siku zilivyokwenda alizidisha upendo wake kwangu. Hakuna nilichohitaji kwake akaninyima, aliwahi kumdanganya baba yake kuwa anaumwa akatumiwa pesa ilimradi anipatie mimi nilipomwambia kuwa kuna mtu ananidai na abananisumbua kwelikweli. Alisikitika kusikia vile, akaahidi kunipigania. Haikuwa kweli nilichomwambia juu ya kudaiwa, pesa ile aliyonipa niliitumia kulipia chumba nikafanya uzinzi na Fatuma. Alihadithiwa habari hiyo na marafiki walioniona nikiingia kule, akalia kwa uchungu mbele yangu, lakini neno lake la mwisho likabaki kuwa ‘NAKUPENDA SANA…..WEWE NI MWANAUME WA MAISHA YANGU’……..Nilij isikia vibaya lakini nafsi nyingine ikanikumbusha kuwa nilikuwa katika mahusiano na msichana yule kwa sababu moja tu…NGONO… na katu hakutaka kushiriki ngono na mimi. Alinikwepa sana hadi nikajisikia vibaya. Nikahisi huenda ana mtu mwingine. Hakika nilidhani kuwa anajihusisha na mtu mwingine ambaye hushiriki naye tendo hilo la ngono ambalo kwangu mimi kilikuwa kitu pekee ambacho kingeweza kuniaminisha kuwa ananipenda kweli. Msichana mrembo kama huyo kamwe asingeweza kuishi bila kufanya mapenzi. Hakika haikuniingia akilini. Wangapi wenye ,ali zao wanamtongoza, yeye ni nani hadi asiingie majaribuni?? Hapana ni uongo mtupu ananiongopea mimi. Nikaendelea na vimbwanga vya hapa na pale. Hakuchoka kunibembeleza, hakuchoka kunipenda na hakuchoka kunikumbusha kuwa ni mimi pekee nilikuwa katika moyo wake wa nyama. “Nikipotea jumla nd’o utajua kuwa nilikuwa nakupenda..” aliwahi kunambia neno hilo. Japo lilinigusa lakini sikulitilia maanani. Hatimaye tukamaliza shule, nikategemea kuwa ule muda wa kumfaidi msichana yule kingono ulikuwa umewadia. Lakini haikuwa hivyo, akaendelea kuwa mgumu huku akijitetea kwa sababu zisizokuwa na kichwa wala miguu. Mwanzoni nilidhani kuwa aliogopa kufanya mapenzi kabla hajamaliza shule, lakini ajabu hadi tulipomaliza bado alisimamia msimamo. Sasa nikajikuta katika pepo mbaya, nikaanza kumwonyesha hadharani kuwa nina wanawake wengine. Japo chozi lake liliniumiza sana lakini sikujali. Kwa nini ananinyima penzi binti huyu? Nilijiuliza. Hatimaye nikafikia uamuzi wa kuachana naye. Lakini siwezi kuachana naye bila kumjua ladha yake. Nilijiapia kuwa jambo hilo haliwezekani hata kidogo, mimi kama mwanaume kamili atanitangazaje kwa marafiki zke, kuwa sijawahi kulala naye tukafanya tendo??? Aibu kubwa!!! Nikampangia shambulizi moja la mwisho na kama ni ubaya uwe ubaya tu. Ilimradi nilishapanga kuachana naye….haitanidh uru lakini lazima nifanye naye tendo Nilimuita nyumbani kwangu, ilikuwa mida ya jioni. Alipofika nilimlaghai hapa na pale nikamgusa matiti yake madogo yaliyosimama wima yakijitahidi kunidhihaki. Na yalifanikiwa hasa hasa kunikebehi. Nikamgusa huku na kule..nilipotak a kumvua nguo akanizuia. Nilikuwa nimekunywa pombe kiasi hivyo sikuwa na aibu, nikaamua kutumia nguvu, niliamua KUMBAKA…..nikai chana sidiria yake, kisha nikaiondoa chupi yake sasa akabaki yu uchi wa mnyama. Alihaha huku na kule asiamini kile kinachotokea mbele yake. Nikamrukia ili niweze kutimiza lengo… Kamwe sikuwahi kumwona binti huyu akiwa katika uoga namna ile…alikuwa amekodoa macho yake….na alikuwa anatetemeka… Akataka kukimbia uchi, nikamdaka mkono nikamvutia pale nilipokuwa. Sikuwa nahuruma hata kidogo, nilichotaka ni itu kimoja tu..NGONO KISHA AKINICHUKIA NA ACHUKIE. Mara akatokwa na kelele kubwa sana zilizonishtua sana. Amakweli sikuzitegemea. Sikudhani kama amnaweza kufanya tendo lile “ANANIBAKAAAAA, NISAIDIEENI ANANIBAAAKA…..” ilikuwa kelele kubwa haswa, na alifanya kwa kurudia rudia Kelele zikawafia wasamalia wema, binti akaendelea kupiga kelele. Hatimaye mlango ukavunjwa, wasamaria wakanivagaa na kuanza kunipiga……nilip igwa hadi nikapoteza fahamu. Nilipozinduka nilijikuta na pingu mkononi, pingu iliyounganishwa na kitanda. Nilikuwa na maumivu makali mwili mzima. Nikakumbuka kuwa nilifumaniwa nikitaka kufanya ubakaji. Pombe zilikuwa zimenitoka na niliona aibu wa kitendo cha kinyama nilichotaka kumfanyia Maria. Baada ya kujitambua vyema na nguvu kunrejea mwilini nilirejeshwa mahabusu. Nikaingia mahabusu nikikabiliwa na kesi mbaya ya ubakaji. SIKU NNE baadaye nilikuja kutolewa……hapak uwa na dhamana lakini ilikuwa barua tu ya kustaajabisha niliyokutana nayo. “Mpenzi Christopher mwanaume wa maisha yangu…..haikuwa nia yangu kukusababishia kipigo kikali na kuitwa mbakaji… nimefan ya haya kwa sababu nakupenda kutoka moyoni…napenda uishi miaka mingi..Chriss ni wewe mwanaume pekee niliyetokea kuvutiwa naye kihisia ukauteka moyo wangu na kujikuta nikiwa mtumwa wa mahaba yako… lakini nina mapungufu makubwa…nina kasoro kubwa ambayo hainipi hadhi ya kulala kitanda kimoja na wewe…..Chriss mimi ningekuwa muuaji iwapo ningekuruhusu unibake….hivi chriss unadhani mpapaso wako haukunisisimua? Nilisisimka haswa na nilitamani nikutimizie kwa hiari kile ulichotaka, labda mimi nilikuwa muhitaji kuliko wewe mpenzi lakini…..lakini nisingeweza kukuua, ….Chriss ninayo furaha na wala usisikitike kusikia hili, mimi nimefurahi sana kufa nikiupigania uhai wa mwanaume niliyempenda, ninayempenda na ninayekufa kwa ajili yake. Kitanzi hiki kiwe kumbukumbu yako milele kuwa NILIKUPENDA…….C hriss mimi ni muathirika wa gonjwa la UKIMWI niliambukizwa na wazzi wangu …nilizaliwa nikiwa na Ukimwi Chriss, mama kabla ya kufa alinikanya kuwa nisiwe na tabia kama ya marehemu baba ambaye alimuambukiza maksudi kutokana na taba yake ya kutotulia nyumbani, mama akanikanya kuwa ni heri nife peke yangu kuliko kuua yeyote asiyekuwa na hatia. Na huyo mtu ni wewe Chriss haukuwa na hatia na haukustahili kufa..…..laiti kama ungenibaka basi leo hii ningekufa nikiwa MUUAJI… ninafura hi kuwa nakufa kama SHUJAA. Nimeyaadika haya huku kitanzi kikiwa shingoni mwangu, nakufa leo lakini wakuache wewe huru. Huru kabisa, naenda kuungana na mama yangu nimweleze kuwa sikuwahi kuua duniani na nimeamua kuondoka ili siku moja nisije kuua yeyote. Ubaki salama Chris wangu” Nilijikuta napoteza fahamu tena baada ya kuhakikishiwa kuwa Maria alizikwa baada ya kujinyonga katika chumba chake nyumbani kwao nabaruaile ilikutwa chini ya miguu yake iliyokuwa unaning’inia……. nilipozinduka nilikuwa nyumbani kwetu…kila jicho lilinitazama kwa namna yake……wengine kwa hasira wengine dharau na baadhi kwa huzuni. AMA KWA HAKIKA nilikuwa na mpenzi aliyenipenda kwa dhati……. UPUMZIKE PEMA PEPONI Maria…..kamwe sitakusahau mpenzi……. UJUMBE; Usilipize baya kwa baya kwa kizazi kisichokuwa na hatia…..JIFUNZE kupenda kwa dhati lakini HISIA ZAKO ZISIKUFANYE MTUMWA!!!!

 SHARE KWA WENGINE MWISHO!

Monday 11 April 2016

MADUKA ZAIDI YA 150 YAUNGUA MOTO!!!


Moto mkubwa umezuka na kuteketeza vibanda vya madukazaidi ya 150 katika mji wa Kayanga wilaya ya Karagwe mkoawa Kagera magharibi mwa Tanzania. Moto huo ambao ulianza Jumatatu majira ya sa 2:00 usiku umeteketeza mali na bidhaa za aina mbalimbali kama mchele, sukari, nguo, simu, pamoja na bidhaa zingine.Gloria Kilio ambaye alikuwa akiuza vyakula vya nafaka, amesema stoo zake zote tatu (3) za nafaka zimeungua, “Stoo zilikuwa na magunia ya unga, mchele na sukari lakini vyote vimeteketea,” amesema Gloria huku akilia. Anasema wakati moto unatokea alikuwa tayari amekwisha kwenda nyumbani na kuwaacha wafanyakazi wake wakimalizia kufunga vibanda.Wafanyabiashara wengi wanasema walikuwa na mikopo nawengi wao hawana bima ya mali zao. Jonasi Nyarugenda ni miongoni mwa wafanyabiashara hao: “Moto umeteketeza stoo zangu nne zenye bidhaa mbalimbali kama sukari, mchele, ngano na mafuta,: anasema Jonas na kuongeza, “kwakeli ukitathimini kwa haraka siyo chini ya milioni 45 zimepotea.” Amesema kwamba alikuwa hana bima katika mkopo wake wa milioni 20 kutoka katika benki.Hasara hiyo kwa kiasi kikubwa imechangiwa na ukosefu wavifaa vya kuzima moto. Wananchi wa Karagwe imewapasa kusubiri gari la Zimamoto kutoka Bukoba Mjini (magari ya uwanja wa ndege) ambako ni kilomita 120 kufika karagwe mjini. Hata hivyo magari hayo yalikuta maduka mengi yamekwishateketea.Diwani wa kata ya Kanoni wilaya karagwe Sabi Rwazo amesema tukio hilo limewastua na ni tukio la kwanza la moto kuunguza soko wilayani humo. Anasema tatizo la ukosefu wa gari la zima moto linachangiwa na uhaba wa fedha. “Mara nyingi katika bajeti yetu imekuwa ikishindwa kununua gari.” Amesema Rwazo na kusema maombi yao yako serikali kuu.Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Deodatus Kinwiro amesema kuwa Serikali ya wilaya yake itapata gari la zima moto hivi karibuni, “Bahati nzuri nilikuwa Dar es Salaam, nimekutana na kamishna mkuu wa zima moto ameniahidi kunipatia gari jipya,” amesema Kinwiro na kuongeza kuwa, “wakati wowote gari hilo litafika wilayani Karagwe.”Hata hivyo baadhi ya wananchi wanasema hawakubaliani na kauli hiyo ya mkuu wa wilaya kwa sababu wamekuwa wakitozwa kiasi cha TZS 30,000 kwa mwezi ili kuchangia huduma za zimamoto wilayani hapo lakini wanashangaa kwa nini hawapati elimu ya kujikinga na majanga, na hakuna hata gari la dharura.Mpaka sasa chanzo cha moto huo hakijajulikana lakini taarifa za awali zimeonesha kuwa kuna Mamalishe mwenyekibanda sokoni hapo aliacha jiko lake bila kuzima hivyo likashika nguo zilizokuwa katika kibanda hicho na kusababisha moto kusambaa ghafla.

Friday 8 April 2016

HUWEZI AMINI!!!MBWA ANUNULIWA VIATU NA VIFAA VINGINE VYA KISASA😂😂😂


MBWA mwenye umri wa miaka saba anayeitwa Scooby ni miongoni mwa mbwa 35 maarufu wanaotumiwa na Jeshi la Ulinzi la Uingereza amenunuliwa vifaa malum vya kumkinga hasa awapo kazini.

Scoobyamenunuliwa miwani maalum ambayo itamsaidia kuzia vumbi kuingia machoni, viatu maalum kuzui miba na vitu vingine vinavoweza kumletea madhara awapo kazini pamoja headphone maalum kwa ajiri ya kunasa sauti mbalimbali zikiwemo za wahalifu na waongozaji wake.

Scooby ni miongoni mwa mbwa wakongwe kwenye kambi ya Jeshi ya Jeshi kikosi maalum cha mbwa (105 Military Working Dog Squadron). Amefanya kazi kwa miaka mitano tangu 2012 kwenye mapigano ya Afghanistan. Kazi yake kubwa ni ukaguzi wa mizigo, vyombo vya moto na kunusa ili kutambua kama kwenye kuna madawa ya kulevya.

Vifaa hivyo vitamsaidia wakati wa mafunzo maalum ya miezi mitatu nchini humo. “Mbwa huyo hang’ati hovyo. Amefundishwa vizuri na amezoea mazingira hasa ya kazi.” Alisema Steve Hood ambaye ni mkufunzi wa mbwa

Wednesday 30 March 2016

NI AJABU KWELI!!!JIONEE NAMNA WATU WANAVYOWEZA KUZIBADILI HISIA ZA KISASI NA KUWA ZA KINDUGU

Pamoja na kuwa na uhasama mkubwa sana kati yao,Babu huyu raia wa afghanistan alikutwa akimpa mwanajeshi huyu wa marekani kikombe cha chai.Hii ni ishara ya UPENDO na kuthamini watu wengine pia.Dada mmoja ambae alikuwa na wenzie katika mashindano ya kukimbia mita 3200 aliamua kusimama na kumsaidia mwenzie aliekuwa ameumia ili kumaliza mbio.Japo walimaliza nafasi ya 14 na 15 lakini wote wawili walipewa tuzo maalumu ya heshima.Japo kulikuwa na vita kali sana inayoendelea,Mwanajeshi huyu muungwana aliamua kumchukua mbwa mmoja ambae alikuwa akiwafuatilia nyuma kwa umbali mrefu sana.Hatimae mwanajeshi huyu alimtoa mbwa huyo sehemu ya mateso na kumfikisha sehemu salama.Wakati wa maandamo yaliyotokea nchini Misri mwaka 2011 watu hawa hapa chini ni WAKRISTU waliokuwa wakiwalinda wenzao WAISLAMU waweze kufanya ibada vema.WAISLAMU pia walifanya vivyo hivyo kwa WAKRISTU.Ni dalili ya utu wema.Baada ya kutokea kwa kimbunga na upepo mkali katika jiji la New York nchini Marekani,sehemu kubwa ya jiji hilo iliharibika sana hasa ile ya nishati kama umeme na miundo mbinu mingine kama barabara.Katika picha wanaonekana watu wakitoa msaada wa kuchajisha simu kwa wale waliokosa huduma ya umeme.Daima tujifunze utu na kusaidia wengine pia.Share kwa wengine kama umeupenda UTU wao.Pia wasamehe na kuwajali adui zako pia.

Tuesday 29 March 2016

JIONEE WATU WENYE UWEZO WA AJABU NA KUSHANGAZA


Je unafahamu kuwa watu wenye nguvu za ajabu kuliko uwezo halisi wa kibinadamu wapo?Ni kweli watu hao wapo na wengine wanaishi hadi sasa.Ni watu ambao wana vitu vya ajabu kama uwezo,nguvu na kuwa imara madhubuti.Wafuatao ni baadhi ya watu hao

1.WIM HOF
Huyu ana uwezo wa kukaa muda  mrefu sana eneo la baridi kali sana bila kupata madhara yoyote yale.Huyu ni mtu halisi anaweza kukaa muda mrefu sana eneo la baridi kali sana.Anazo tuzo 21 za Guinness ikiwemo ya kuoga kwenye maji ya barafu kwa muda mrefu.Huyu anaweza kukaa kilele cha mlima kilimanjaro kifua wazi kwa muda mrefu.

2.KELVIN RICHARDSON
Huyu ana uwezo mkubwa sana wa kuwaelewa wanyama.
Ana uwezo mkubwa sana wa kufanya urafiki hata na wanyama wakali zaidi duniani bila tabu yoyote.Ana uwezo wa kuwa na urafiki na chui,simba na fisi.Huwafanya marafiki na hata kulala nao pia.

3.CLAUDIO PINTO
Huyu anajulikana kama MACHO YA DARUBINI.Ana uwezo wa kuyatanua macho yake kipimo cha 7mm ambapo ni kiasi cha 95% ya mzunguko wa jicho lake.

4.HAROLD WILLIAMS
Anajulikana kama MWALIMU WA LUGHA.Huyu anasifika kwa kuwa na uwezo wa kujua lugha nyingi sana duniani.Je wewe una uwezo wa kujua lugha ngapi katika maisha yako yote?Huyu anafahamu lugha zaidi ya 58 ambazo anaziongea na kuandika bila shida yoyote ile.
Sio peke ake alie na kipaji hiki,pia wapo John Browning,Joseph Caspar na Doktar Carlos do Amaral Freire.

5.TIBETAN MONKS
Wana uwezo wa kuweka sawa JOTO la miili yao kwa kutumia akili au ufahamu wao.Wana uwezo qa kubadili joto la miili yao kwa kutumia akili yao tu.Wamewahi kurekodiwa wakibadili jotoridi lao kufikia kiasi cha nyuzi joto 8 za sentigredi.

6.RATHAKRISHNAN VELU
Anajulikana kuwa na meno ya ajabu yenye nguvu sana maarufu kama 'steel teeth'.Ana uwezo wa kuvuta treni ya mabehewa saba akitumia meno yake kuivuta kwa kutumia kamba ya chuma.Anajulikana pia kwa jina la KING TOOTH.

7.DANIEL BROWNING SMITH
Huyu anajulikana kama 'The rubber boy' ana uwezo wa kujipinda zaidi katika mikao mbali mbali.

8.STEPHEN WILTSHIRE
Ana uwezo mkubwa sana wa kukumbuka.Huyu ana uwezo wa kutazama kitu mara moja tu na kuweza kukichora kwa ufasaha kabisa.Ni maarafu sana kwa kuchora picha za miji mbali mbali kwa kuiangalia mara moja tu.Kama watu wengine hutizama mara kwa mara katika uchoraji huo,yeye hutizama mara moja tu na kuchora sehemu kubwa ya mji husika.

9.JESUS ACEVES
Huyu ni mtu mwenye nywele nyingi zaidi za usoni.Anapatikana katika familia ya kimexico yenye wanafamilia 24 ,huwa anazunguka duniani kuonesha watu muonekano wake huo.

10.DANIEL TAMMET
Ni mtaalamu sana wa mahesabu na hesabu kwa ujumla.Hufanya kwa kutumia akili yake hesabu nzito nzito tena kwa speed ya hali ya juu sana.Pia ana uwezo wa kuongea lugha saba bila shida.

11.GARRY TURNER
Je ngozi yako ina uwezo wa kujivuta kwa kiasi gani?Kutana na jamaa huyu ambae ngozi yake hujivuta kama mpira.Huivuta ngozi yake kwa namna mbali mbali.Hii inatokana ngozi yake kupungua 'Collagen'

12.NOORSYAIDAH
Ni mwanamke wa kiindonesia ambae anasema kuwa mwili wake una tabia ya kuota waya kwa muda usiopungua miaka ishirini sasa.
Waya hizo huwa kiasi cha sentimita 10 hadi 20.

13AL HERPIN
Kqa kawaida baada ya kukaa siku chache bila kulala kabisa mwili HUZIMIA.Lakini kwa mtu huyu AL,hajawahi kabisa kulala katika maisha yake na hivi sasa ana miaka 94.
Wanasayansi wanaamini kuwa inawezekana hali hiyo ilisababishwa na jeraha alilopata mama yake siku chache kabla ya kumzaa.

14.LIEW THOW LIN
Anajulikana kama MAGNETIC MAN,raia huyu wa Malaysia ana uwezo wa ajabu sana amabpo mwili wake una uwezo wa kuvuta vitu vya chuma.


Saturday 26 March 2016

IJUE HISTORIA YA PASAKA NA MAANA YAKE...



Pasaka ni jina la sikukuu muhimu katika dini za Uyahudi na Ukristo . Jina la Pasaka limetokana na neno la Kiebrania " פסח " (tamka: pasakh).
Pasaka ya Kiyahudi ni sikukuu ya kumbukumbu kwa kutoka kwa Wanaisraeli kutoka Misri wakati wa Musa mnamo miaka 1200 KK.

Pasaka ya Kikristo ni sikukuu ya kukumbuka kufufuka kwake Yesu Kristo siku ya tatu baada ya kusulibiwa kwake. Inahesabiwa kuwa sikukuu muhimu kabisa katika Ukristo.
Taarifa za Agano Jipya zinatoa habari ya kuwa kifo na kufufuka kwa Yesu yametokea wakati wa sikukuu ya Pasaka ya Kiyahudi. Kwa hiyo jina la sikukuu hiyo imeendelea kutumikwa kwa ajili ya sherehe ya kikristo.
Tarehe ya Pasaka

Pasaka ni sikukuu inayobadilika tarehe yake katika kalenda ya kawaida kila mwaka.
Pasaka ya Kiyahudi inafuata kalenda ya Kiyahudi ni tarehe 15 Nisan ambayo ni siku baada ya mwezi mpevu wa kwanza baada ya sikusare ya machipuko (mnamo 21 Machi).
Pasaka ya Kikristo inaunganisha siku ya Jumapili (ni jumapili kila mwaka kwa sababu hii ni siku ya ufufuo katika mapokeo ya kikristo) pamoja na kumbukumbu ya pasaka ya Kiyahudi. Tangu mtaguso wa Nikea Wakristo walipatana kusheherekea Pasaka kwenye
jumapili ya kwanza baada ya mwezi mpevu unaotokea baada ya sikusare ya 21 Machi. Kwa hiyo

Pasaka inaweza kutokea kati ya 22 Machi hadi 25 Aprili.
Tangu masahihisho ya kalenda ya Juliasi na kuanzishwa kwa kalenda ya Gregori mara nyingi kuna tofauti kati ya Pasaka ya kimagharibi (kanisa katoliki na makanisa ya kiprotestanti) na Pasaka ya Kimashariki ya makanisa ya Kiorthodoksi kwa sababu Waorthodoksi wanaendelea kutumia kalenda ya Juliasi kwa ajili ya kukadiria sikukuu zao.

Majina ya Pasaka ya Kiyahudi na Pasaka ya Kikristo katika lugha mbalimbali
Katika lugha nyingi asili hii bado inaonekana ingawa mara nyingi umbo la neno ni tofauti kidogo. Jina la sikukuu ya Kiyahudi linapatikana kwa umbo mbalimbali. Siku hizi mara nyingi umbo la neno la Kiebrania limetumika lakini desturi katika lugha hizo inaonyesha pia umbo linalofanana zaidi na neno kwa ajili ya sherehe ya Kikristo.

Friday 25 March 2016

TUMIA MUDA WAKO KUSOMA KISA HIKI CHA KIMAPENZI CHENYE KUELIMISHA NA MAFUNZO TELE!!!!



1st year
nikiwa nimekaa leacture room nikimuangalia msichana aliyekaribu yangu,niliyekuwa nikimuita "Bestfriend"nilikuwa nikimuangalia nywele zake nzuri na sura yake ya upole huku nikitamani awe wangu,lakini yeye hakuwa akitamani hilo na nilikuwa nikilitambua hilo.
Baada ya leacture,alikuja kwangu na kuniomba notes za siku ya nyuma kwa sababu hakuweza kuingia darasani hiyo siku iliyopita.baada ya kumpa akasema "asante" na kushikana mikono na mimi.I wanted to tell her,i want her to know that i don't want us to be just friends,i love her but i'm just to shy,and i don't know why
2nd year
Simu yangu iliita,kupokea alikuwa yeye alikuwa akilia akinielezea jinsi gani boyfriend wake broke her heart,she asked me to come over because she didn't want to be alone,kwa kuwa ni rafiki yangu kipenzi ilinibidi kwenda kumfariji,as i sat next to her on the sofa,nilikuwa nikimuangalia Machoni nikitamani awe wangu.Baada ya masaa mawili baada ya kuangalia nae movie mbili tatu na kula nae chakula pamoja akarudi katika hali yake ya kawaida,hivyo akaamua kwenda kulala,before akaniangalia na kuniambia "asante" na kunipa tabasamu tamu,i want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why.
3rd year
Siku moja kabla ya Tamasha la muziki chuoni alikuja kwenye meza yangu leacture room na kuniambia "Boyfriend wangu amepata udhuru hivyo naomba unipe campan katika tamasha la muziki leo usiku" kwa kuwa tuliwekeana promice kwamba ikitokea kila mmoja wetu amekosa mtu wa ku-date nae basi tutaenda pamoja just as "bestfriends".hivyo tukaenda.
katika tamasha baada ya kila kitu kuisha na muziki kufungwa,nilikuwa nimekaa nje ya ukumbi nikimuangalia jinsi alivyokuwa akicheka na rafiki zake,she saw me looking to her she smiled at me,i want her to be mine lakini yeye alikuwa hafikirii hilo kabisa na nilikuwa nikilitambua hilo,then she said to me "nimekuwa na muda mzuri na wewe asante sana" and she gave me a sweet smile.I want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why.
Graduation Day
siku,wiki kisha mwezi ukapita ilikuwa ni mahafali yetu tukimaliza masomo ya chuo,akiinuka kwenda kutunukiwa shahada yake ya uchumi nilikuwa nikimuangalia akiwa amependeza sana siku ile,i wanted her to be mine,but she didn't notice me like that,and i knew it.
kabla watu hawajatawanyika kwenda makwao,alikuja kwangu akiwa na vazi lake la mahafali,na kulia pale nilipomkumbatia akainua kichwa chake na kuniambia "you are my bestfriend asante sana" i want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why.
Miaka michache baadae
Nikiwa kanisani Yule Msichana akiwa anaolewa sasa,nilimuangalia akisema "ndiyo nakubali " and drive off to new life,kaolewa na mwanaume mwingine,i wanted her to be mine,but she didn't see me like that,and i knew it.
but before she drove away,alikuja kwangu na kusema "asante sana" and kissed me on the cheek.I want to tell her to know that i dont us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why.
Kwenye Mazishi
Miaka ilipita i looked down katika jeneza lilokuwa na msichna ambaye alikuwa ni "bestfriend" wangu,Katika Service ya mazishi wakasoma diary ya Bestfriend ambayo alikuwa akiiandika enzi za maisha ya chuo'
Diary yake ilikuwa Ilikuwa ikisomeka hivi
I stare at him napenda awe wangu,but he doesn't notice me like that,and i know it,i want to tell him,i want him to know that i dont want us to be just friends,i love him but i'm just to shy,and i dont know why.I wish he would tell me he loved me!
Nilipiga magoti huku nikilia nikijisemea moyoni i wish ningemwambia tu ukweli,nimeshachelewa sipo nae tena katangulia mbele za haki i cried!!
Vunja ukimya

Thursday 24 March 2016

KUTANA NA DOGVINCI,MBWA MAARAFU KWA UCHORAJI


Sio tu binadamu wenye uwezo wa kufanya mambo makubwa na ya ajabu.Hata wanyama wana uwezo wa kufanya mambo mengine tena katika kiwango kikubwa zaidi ya binadamu.

Mbwa anaeitwa Dagger amekuwa mchoraji maarufu sana baada ya kufundishwa na mlezi wake Yvonne.

       "Mara nyingi amekuwa akiniangalia sana wakati nachora hadi akapata hamu ya kujifunza.Baadae akaanza kunisumbua sana na nikamuuliza unataka kuchora?Akaanza kutingisha mkia kama ishara ya kukubali.Nikamwambia sawa"
Alisimulia Yvonne akihojiwa na gazeti la ABC 7New York.

Baada ya kutumia muda kumfundisha mbwa huyo,hivi sasa anaitwa DOGVINCI pale New York kutokana na uchoraji wake wa hali ya juu.

Michoro ya mbwa huyo inauzwa kati ya dola $20 hadi $200 za kimarekani kwa mchoro mmoaja.Faida kubwa inayopatikana inapelekwa kwenye organization ya "Canine Companions for Independence".
Ama kweli haya ni maajabu!!!!!Jionee picha zaidi


Wednesday 23 March 2016

YAJUE MADHARA YA KUVAA NGUO PENDWA ZA KUBANA SANA MWILI!!!


Mbali na ukweli kwamba baadhi ya mitindo ya mavazi inasababisha adha kubwa kwa watumiaji, mitindo mingine husababisha atharimbaya kwa afya kwa watumiaji na jamii kwa ujumla.Miongoni mwa mitindo ya mavazi inayosababisha athari mbaya za kiafya ni ile ya mavazi yanayobana sana.

Tafiti kadhaa za kisayansi zinabainisha kuwa miongoni mwa nguo zinazoathiri afya ni nguo za ndani za wanaume zinazobana sana maarufu kama kama boksa pamoja na suruali za jeans zinazobana maarufu kama ‘skinny jeans’ ambazo mara nyingi huvaliwa na wanawake.Nguo zinazobana sana husababisha mishipa midogomidogo inayosafirisha damu kubanwa na kuathiri usambazaji wa damu kwenye baadhi ya maeneo ya mwili.Kutokana na hali ya kubana, nguo hizo husababisha uharibifu wa misuli na mishipa ya fahamu katika mapaja na miguu hasa kwa wanawake.

Mara nyingi madhara ya nguo hizi hujitokeza kama dalili ya miguu kufa ganzi au hisia za miguu kuwaka moto na ni mara chachewahusika kutambua kuwa dalili hizo chanzo chake ni mavazi.Katika ripoti ya hivi karibuni iliyochapishwa Juni mwaka 23, mwaka jana na Jarida la Neurology, Neurosurgery and Psychiatry, inaonyesha kuwa watafiti katika Hospitali ya Royal Adelaide nchini Australia walihusisha nguo za kubana sana za aina ya jeans na kutokea kwa tatizo la misuli lijulikanalo kitabibu kamacompartiment syndromeambalo alilipata mwanamke mmoja nchini humo.“Ugonjwa wa mwanamke huyu unaonyesha madhara mapya ya uvaaji wa jeans zinazobana.”  alisema

Dk Thomas Kimber, mmoja wa watafiti waliotoa ripoti hiyo alipokuwa akizungumza kuhusu madhara ya mavazi ya kubana.Mtaalamu wa mishipa ya fahamu na mwanachama wa chama cha Madaktari wa Mishipa ya Fahamu cha Marekani (AAM), Dk John England, anasema:

“Mishipa ya fahamu kwa baadhi ya watu, inaweza kukandamizwa kwa urahisi. Mshipa wafemoral cutaneousunaotoka kwenye nyonga na kuingia mapajani kwa ajili ya kuchukua hisia, unaweza kubanwa na kitu chochote kinachobana mapaja au eneo la kiuno.”

Hali ya kubanwa kwa mishipa ya fahamu kama itakuwa ya kujirudia rudia inaweza kusababisha madhara ya kudumu.Madhara ya nguo za kubanaKwa wanawake nguo zinazobana kupita kiasi zinaweza kusababisha damu kuganda ndani yamishipa, uvimbe wa mishipa ya damu kwenye miguu na magonjwa ya fangasi ya ngozi yanayoambatana na muwasho.Hii inaweza kutokea kwa sababu ya jasho linalozalisha kwa wingi katika nguo zinazobana na kufanya ngozi ikose hewa safi.Uvimbe wa mishipa ya damu miguuni maarufu kama vericose veins, ni moja ya matatizo yanayowapata mara kwa mara wanawake wajawazito na wale wanaotumia vidonge, vipandikizi na sindano za kupanga uzazi bila kufanya mazoezi ya mwili.

Tatizo jingine kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa mwaka 2004 katika toleo namba117(2) la Jarida la Ejog (Europian Journal of Obstetrics & Gynaecology and Reproductive Biology) ni ongezeko la kuzaliana kwa bakteriawaharibifu ambao wanasababisha mwanamke kutokwa na usaha katika sehemu za siri.Hali inaweza kuwa mbaya zaidi kwa wanawake wanene na watu wenye tatizo la ugonjwa wa kisukari.Kwa wanaume, mavazi haya yanaweza kuathiriutendaji wa figo pamoja na kibofu cha mkojo na kuchochea kutokea kwa maambukizi katika njia ya mfumo wa mkojo.Yanaweza pia kusababisha uvimbe wa mishipa ya korodani au makende na kuathiri ubora wa mbegu za kiume. Hali hii wakati mwingine huwani chanzo cha ugumba na upungufu wa nguvu za kiume kutokana na athari za maumbile ya kianatomi pamoja na athari za kisaikolojia.

Utafiti ulioongozwa na Dk F. Parazzini wa nchini Italy na kuchapishwa mwaka 1995 katika Jarida la International of andrology toleo namba 18(3), ulionyesha kuwa, uvaaji wa nguo zinazobana unaathiri uwezo wa wanaume kuzalisha mbegu za kutosha.Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake naUzazi katika Hosipitali ya Taifa Muhimbili, Dk Cyril Massawe anasema athari za mavazi hayayapo mengi na mbaya zaidi ni yale yanayogandamiza mfumo wa uzazi wa mwanaume. Anaonya kwamba watu wengi wanaovutiwa na mavazi hayo hasa vijana, wanapaswa kuwa makini kwa sababu tafiti zilizofanywa zimethibitisha watu kuathirika.

“Mwanaume ili kuhifadhi vizuri mbegu zake, anatakiwa kutumia mavazi yenye kupitisha hewa,” anasema Dk Massawe.

Kutokana na athari za muda mfupi na zile za muda mrefu za mavazi yanayobana sana mwili, mtaalamu huyo wa afya anaonya jamii haina budi kuzingatia afya na usalama kwanzakabla ya kufikiria urembo na kupendeza.

“Ni muhimu kukumbuka kuwa urembo na utanashati bila afya njema ni sawa na kujificha katika kichaka cha karanga,” anaonya kwa usemi huo wa Kiswahili.

Karanga ni mmea unaoota kwa mfano wa kichaka lakini urefu wake hauzidi sentimita 20 hivyo hauwezikumsitiri mtu, ili ajifiche, asionekane.

Je, tabia hii yaweza kukoma?Ni vigumu kubadili mitindo ya mavazi ambayo inashabikiwa hasa ikizingatiwa kuwa athari zake si za wazi. Mtu anaweza kusema kuwa amevaa mavazi ya namna hiyo kwa muda mrefu lakini hajaona madhara. Lakini ukweli ni kwamba athari zake zinaweza zisionekane wazi lakini zikawa ni za polepole na ambazo zitasababisha madhara makubwa miaka ijayo.Suala la kubadili tabia ni la mtu binafsi na ni jambo ambalo litatokana na mhusika baada yakupima faida na madhara ya mavazi haya yanayopendwa zaidi.

Ni suala la mtu kujiuliza; nionekane mtu wa kisasa kwa wakati huu mbele za watu na baadaye niwe na matatizo ya kiafya au niachane na mambo ya kuiga ili niwe na afya njema maishani.Kuonekana nadhifu na mtanashati siyo lazimakuvaa mavazi yanayobana sana. Waweza kuvaa mavazi yanayoruhusu mwili kutoathirika na ukaonekana nadhifu.Tatizo hapa ni ile hali ya kuvaa mavazi yanayobana mwili na wengine ingawa wanajihisi vibaya huvumilia. Kumbuka kuwa na afya bora kwa sasa na siku za baadaye za maisha yako ni jambo muhimu katika kukufanya uishi miaka mingi duniani.