Friday 3 June 2016

BONDIA MAARUFU MUHAMMAD ALI AFARIKI DUNIA.



Aliekuwa bondia maarufu duniani,Muhammad Ali amefariki kwa mujibu wa msemaji wa familia yao.Ali amefariki akiwa na umri wa miaka 74.

Bingwa huyo wa mara tatu wa dunia alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa tangu mwaka 1984 miaka mitatu baada ya kustaafu mchezo wa masumbwi.

Siku moja kabla ya kukubwa na umauti,Ali,alipelekwa hospitali ya Phoenix,Arizona akiwa na matatizo ya upumuaji.Tatizo hili lilipelekea matatizo ya neva za fahamu yaliyoathiri pia mfumo wake mzima wa upumuaji.

Mazishi yake yatafanyika katika mji aliozaliwa wa Louisville,Kentucky.
 
         "Familia ya Ali inapenda sana kuwashukuru sana kwa mawazo,sala na sapoti mliotuonyesha kwa kipindi chote cha kumuuguza Ali"Alimalizia msemaji wa familia.

Rest in peace MUHAMMAD ALI,THE BEAST


Asante kwa kutembelea ukurasa huu.

Share kadili uwezavyo.

No comments:

Post a Comment