Wednesday 18 May 2016

KIJANA WA MIAKA 31 AZAMIA KATIKA PENZI LA BIBI WA MIAKA 91.


Kila mmoja anaamini kuwa umri ni namba tu katika mapenzi.Kama unampenda mtu umri wake hauna nafasi katika mapenzi yenu.Je ni kweli imani hii ina ukweli ndani yake katika kila penzi??

Kutana na Kyle Jones 31,ambaye yuko katika penzi la dhati na bibi kizee mwenye umri wa miaka 91 anaemzidi takribani miaka 60 kijana huyo.Unaweza kusema Kyle yuko katika mapenzi na mtu ambae anapaswa kumwita BIBI.

Kyle anasema anampenda sana MPENZI BIBI huyo ambae tunaweza sema SUGAR BIBI kwa lugha ya vijana wa town.

SHARE NA WENZIO WAPATE HABARI HII.

@viroshare

Wednesday 11 May 2016

IJUE NYOTA YAKO NA TABIA ZAKE


Unajimu au astrolojia ni elimu juu ya uhusiano kati ya nyota na maisha ya binadamu duniani. Wanazuoni wa unajimu wanaeleza ya kwamba nyota zinaathiri maisha ya watu na matukio kama amani, vita au maafa. Mahusiano haya hayajaweza kuthibitishwa na sayansi ya fizikia au sayansi nyingine. Alama za nyota 12 ni msingi wa falsafa hii ya unajimu.
Astrologia imekuwa ikitumika kwa miaka mingi lakini siku zote imekuwa ikipata upinzani mkubwa toka kwa wana sayansi.
Astrolojia ina misingi tokea enzi za zamani wakati sayansi ilipokuwa ya chini na imani za kiroho na kiungu zikiwa za kiwango cha juu katika jamii nyingi.
Baadhi ya tafiti zilizofanywa kuchunguza usahihi wa astrolojia unaonyesha kuna usahihi wa asilimia kama 3o tu. Hii si haba,kuna ukweli basi katika hili japo bado kuna upinzani mkubwa toka katika ulimwengu wa sayansi ya kisasa.
[Soma pia: Madhara ya Mwezi Katika Hisia na Tabia za Binadamu:Kuna Ukweli? , Nyota na Kazi Zenye Mafanikio ]
Tabia Za Watu Na Alama Za Nyota
Alama za nyota zinabashiri tabia na haiba ya binadamu katika dunia. Mpangilio au nafasi ya sayari katika mzunguko wake angani unaaminika kuleta athari kwa binadamu na matukio katika dunia.
Kuna alama 12 za kiastrolojia. Kila moja ina mvuto wa nguvu wa kipekee toka katika nyota.
Alama hizi ni kama ifuatavyo:

1. Samaki (Pisces):Feb 19 – Machi 20
2. Kondoo (Aries): Machi 21 – Aprili 19
3. Ng’ombe (Taurus): Aprili 20 – Mei 21
4. Mapacha :(Gemini ): Mei 22 – Juni 20
5. Kaa(Cancer): Juni 21 – Julai 22
6. Simba (Leo): Julai 23 – Agosti 22
7. Mashuke (Virgo):Agosti 23 – Sept 22
8. Mizani (Libra): Sept 23 – Okt 22
9. Ng’e (Scorpio): Okt 24- Nov 21
10. Mshale (Sagittarius): Nov 22- Des 21
11. Mbuzi (Capricorn):Des 22 – Jan 19
12. Ndoo (Aquarius):Jan 20 – Feb 18

Makundi Ya Alama Za Nyota:
Alama hizi 12 za nyota zinagawanyika katika elementi 4 zijulikanazo kama:
Moto: Yenye matamanio ya mafanikio au makuu,dadisi
Maji: Yenye kubadilika na yenye uwezo wa ufahamu wa ndani
Hewa: Imara na yenye kukuza au kuendeleza
Udongo: Yenye elimu au uwezo wa kutambua na yenye kuhamasisha
Hizi ni elementi nne zinazoongoza astrologia. Kila kimojawapo kinabeba tabia fulani.

Alama hizi 12 za nyota zimegawanyika kama ifuatavyo:
Moto : Kondoo, Simba,Mshale
Maji: Ng’e, Samaki, Kaa
Hewa: Mapacha, Mizani, Ndoo
Udongo: Ng’ombe,Mashuke,Mbuzi

ZIFUATAZO NI NYOTA MBALI MBALI NA TABIA ZAKE







SHARE KADRI UWEZAVYO NDUGU. .ASANTE KARIBU TENA KWA HABARI ZA KIPEKEEE

Wednesday 4 May 2016

TANZANIA YAONGOZA KWA UKUAJI WA UCHUMI EAC

Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu zaidi cha ukuaji wa uchumi wake mwaka huu katika kanda ya Afrika Mashariki na kati.
Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la fedha la kimataifa - IMF.
Katika ripoti yake iliyotolewa hii leo Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu cha ukuaji wa uchumi wake wa asilimia 6.9% mwaka wa 2016.
Kasi hiyo ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania ni ya pili tu nyuma ya Ivory Coast baina ya mataifa ya Kusini mwa jangwa la Sahara .
Ivory Coast inatarajiwa kukuwa kwa kasi ya asilimia 8.5%.
Katika kanda ya Afrika Mashariki ,uchumi wa Kenya ndio wa pili kwa kasi ya ukuaji kwa asilimia 6%.
IMF hata hivyo inasema kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi kusini mwa jangwa la Sahara unatarajiwa kupungua kwa mwaka wa pili mfululizo kutokana na kudorora kwa viwango vya uzalishaji na hivyo uwekezaji.
Kwa mujibu wa shirika la fedha la kimataifa - IMF, eneo hilo linakadiria kushuka kwa ukuwaji wa uchumi kwa asilimia 3 mwaka huu.
Kiwango hicho ni cha chini kabisa kuwahi kushuhudiwa katika miaka 15.
Mataifa yanayotegemea mapato yanayotokana na mafuta ndiyo yalioathirika zaidi kama vile Nigeria na Angola.
Aidha Zambia pia imeathirika vibaya kutokana na ukosefu wa soko la kimataifa la shaba yake.
Ripoti hiyo inaitaja Afrika Kusini kama moja ya mataifa ambayo kiwango chake cha ukuaji kimedorora kwa kiasi kikubwa mno.
Katika orodha ya mataifa yanayotarajiwa kuwa na kiwango cha juu cha ukuaji Kusini mwa jangwa la sahara Ivory Coast ndio inayoongoza.
Orodha ya mataifa ya kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara na viwango vya kasi ya ukuaji wa uchumi 2016.
1. Ivory Coast 8.5%
2. Tanzania 6.9%
3. Senegal 6.6%
4. Kenya 6%
5. Zambia 3.4%
6. Nigeria 2.3%
7. Afrika Kusini 0.6%

Source:bbc

Tuesday 3 May 2016

JINI MAHABA NA NAMNA MAJINI WANAVYOINGIA KATIKA MAISHA YA BINADAM




Majini ni viumbe ambao wameumbwa kwa Moto na walikuwa wakiishi duniani kabla ya binadamu miaka Milioni nyingi iliyopita.
Viumbe hawa wana tabia kubwa mbili;
Yaani ya kibinadamu kwa maana wanakuwa wanafanya mapenzi, wanazaa na wanakufa.
Tabia nyingine ni ya Kimalaika ambayo ni kwamba wana uwezo wa kujigeuza katika umbo lolote wanalotaka na vile vile wanaruka na kwenda wanakotaka au kupita wanakotaka bila kutumia chombo chochote.
Taifa la Majini limegawanyika katika makabila Milioni Sabini na mbili (72,000,000) na wana uwezo wa kujifunza lugha yeyote wanaoitaka.
Idadi ya Majini ni kila Binadamu mmoja kuna Majini 300 na wanaishi katika Majumba yetu, kwenye Miti, Majangwani, Kwenye Mapango na Sehemu zenye Misitu Mikubwa.
Majini wako katika aina Mbili (2); Maruhani na Mashetani.
Maruhani ni Majini wema ambao wanamtii Mwenyezi Mungu na wanawasaidia Binadamu katika mambo mengi.
Mashetani ni Majini Waovu ambao ni wakorofi na wanawaletea Watu madhara na Matatizo mara kwa mara.

Baba wa Majini anaitwa JANN ambaye kimaumbile yeye ana tofauti ndogo na wenzie kwamba yeye ameumbwa kwa ulimi wa Moto.
Pamoja na mambo mengi wanayoyafanya Majini na kujihusisha na binadamu, Majini vilevile wanafanya kazi za Malaika hasa zile za mambo ya kupeleka Habari na kuwalinda Binadamu, mambo ya doria za Angani. Kazi hizi siyo zao lakini kwa vile wanapenda kuiga mambo basi huiga hata kazi ambazo siyo zao.
Majini na Binadamu wana sifa zinazofanana kwani wote wana akili na wote watahesabiwa siku ya Kiama na watazawadiwa kwa mema yao na maovu yao, wote wanakula na kuzaa.
Kama ilivyo, kuna wataalamu wa Kijini wenye fani sawa na Wataalamu wa Kibinadamu wenye kufanya kazi zinazofanana.
Tofauti kubwa iliyopo kati ya Majini na Binadamu ni kwamba; Majini hawana maumbile maalum na wana uwezo wa kujibadilisha katika maumbile mbalimbali ingawa wengi wa Majini wapo katika maumbile ya paka, nyoka na ndege.
Binadamu wao wana umbile maalum ambalo halibadiliki.
Majini wana uwezo wa kuwaingia Binadamu wakati Binadamu hawana uwezo wa kuwaona Majini isipokuwa kwa ufundi maalum.

Namna Majini wanavyowaingia Binadamu iko katika njia tatu:-
1. Njia ya kwanza (1): ni kama Remote Control; Hii inamfanya yule aliyedhibitiwa kuweza kuelewa au kuwa na fahamu zake lakini anakuwa hawezi yeye mwenyewe kuudhibiti mwili wake na anasema yale anayotaka yule Jini.
2. Njia ya Pili (2); Jini humwingia Binadamu ndani ya utosi na kuingia katika Mfumo wa Damu. Hii inamfanya yule Binadamu kupoteza fahamu na anakuwa haelewi kabisa kinachoendlea na anafanya yote anayotaka yule Jini.
3. Njia ya Tatu (3) ni ile ya Jini kukaa nyuma ya Binadamu. Njia hii humfanya yule Binadamu anakuwa hapotezi fahamu ila anakuwa hawezi kufanya lolote na mwili wake.
{mospagebreak}

Majini vilevile wana uwezo wa Kusafiri kwa kasi ya upepo bila kutumia chombo chochote; Binadamu hana uwezo huo isipokuwa kwa msaada wa Majini.
Hiyo ni kusema kwamba mambo yote yanayofanywa na Wachawi na Wanga hayawezekani isipokuwa kwa msaada wa Kijini.
Jambo la muhimu ni kwamba pamoja na uwezo mkubwa walionao Majini, Wanadamu wana uwezo wa Kumtawala na Kumdhibiti Jini na vivyo hivyo Majini nao wanaweza kumtawala na kumdhibiti Binadamu wote kwa kutumia utaalamu maalum.
Wako Majini wa kila Dini na kila Kabila, na kuna watu wanaofuga Majini kwa kujikinga, na kwa kuboresha kazi zao au kujipatia utajiri. Pia kuna watu wanaofunga ndoa na Majini kwa kutumia utaalamu au kwa hiari za Majini hao.
Wabaya wa Majini ni Mashetani ambao wengi hawana Dini na ndio wanaoharibu mimba za Wazazi na kufanya mapenzi na watu usingizini bila hiari zao.
Kuepuka usichafuliwe kimapenzi, kabla ya kulala piga Bismillahi kwa Muislamu au taja jina la Yesu mara tatu kwa Mkristo.

MAUMBILE YAO YAKOJE?

· Majini wana maumbile makuu manne (4);
· Wanakuwa katika maumbile ya Nyoka.
· Wanakuwa katika maumbile ya Nge.
· Wanakuwa katika maumbile ya Mbwa.
· Wanakuwa katika maumbile ya Paka (Mweusi).
· Kuna Majini wengine hawana maumbile yeyote na hawa shughuli yao ni kuruka hewani kuzunguka huku na kule na husafiri mbali kwa mara moja yaani kufumba na kufumbua.

SURA ZA MAJINI NA MASHETANI:
Majini sura zao ni za kutisha na mfano wake ni kama Matunda ya Mti wa Zaqum ambao unatoa matunda yenye sura mbaya na yanayofanana na mawe.
Majini wanakuwa na mkutano kila siku nyakati za kuchomoza na kuzama Jua na nyakati hizo ndizo ambazo wanafanya maasi yao.
Fitna na Maasi yao mengi wanafanyia upande wa Mashariki.
Majini vilevile wanaweza kujigeuza kama mbwa mweusi au paka mweusi kwa sababu Majini wanapenda Rangi Nyeusi kwa sababu ya kiza.

WANAKULA NINI?
Majini wao wanakula mifupa na mavi ya farasi. Hivyo ni vyaluka vyao vikuu pamoja na kwamba wengine wanakula Moshi (Ubani) na wengine wanapenda kunywa damu.
Wanapokula au kunywa, wao hutumia mkono wa kushoto na Majini wazuri ndio ambao wanakula mifupa mizuri na kuwaachia mifupa mibaya na uchafu Majini wabaya au Mashetani.

JE MAJINI WANAZAA?
Majini wanaoa na kuongezeka kama tulivyo Binadamu na huzaana kwa wingi sana.
Katika wao kuna wale wanaokula na kuoana na kuna wale ambao hawafanyi hayo.
Binadamu Mwanamume ana uwezo wa kumuoa Jini Mwanamke na Jini wa Kiume ana uwezo wa kumuoa Binadamu Mwanamke pamoja na kwamba ndoa inayotambulika na Mwenyezi Mungu ni ya kiumbe kwa kiumbe yaani Binadamu kwa Binadamu na Jini kwa Jini.
Huyu ni JINI MAHABA wa Kike anaitwa SUCCUBI huwajia wanaume na kufanya nao Mapenzi
Jini Mahaba wa kiume akiwa Kazini ni hatari sana hawa